Follow us

Ushuhuda: Nilivyowatumia Bundi Kubatilisha Ndoa ya Mtoto wa Shangazi Yangu

Tangazo
Bwana Yesu Asifiwe , jina langu ninaitwa Winnie, mkaazi wa wilaya ya Kisarawe mkoani Pwani.
Kwa sasa nimeokoka na kumpokea Yesu kama Bwana na Mwokozi wa maisha yangu lakini kabla sijaokoka nilikuwa mtumwa wa shetani kupitia uchawi.
Nimeamua kuandika waraka wangu huu baada ya kuguswa .
Ninaona nina wajibu mkubwa wa kuelezea siri hizi za wachawi ili niweze kuwekwa huru lakini pia niweze kuwasaidia watu wengine waweze kuwa huru, kwani maandiko matakatifu yanasema nanyi mtaijua kweli nayo itawaweka huru.
Nimeona si vyema endapo nitakufa nikiwa na siri yangu hii. Mambo niliyo yapitia yamefunza mambo mengi sana maovu yanayo tendeka katika ulimwengu huu ambayo nilikuwa siyafahamu hapo awali.
Ninataka ulimwengu mzima uyafahamu na hivyo kuwa huru.
Nisiwachoshe kwa maneno mengi ila kwa ufupi tu ni hivi mwaka 2014 rafiki yangu mmoja alinipeleka kwa mganga wa kienyeji ili anisaidie niweze kupata mume wa kuniona.
Nilifikia uamuzi huu baada ya mwanaume alie kuwa anataka kunioa kufariki ghafla kwa ajali ya gari huku akiniacha na kichanga cha minane tumboni.
Tukio hilo lilini huzunisha sana kwa sababu mwaka huo wa 2014 nilikuwa nimetimiza umri wa miaka 40 nikiwa bado naishi nyumbani kwa wazazi wangu huku nikiwa na watoto wawili huku kila mmoja akiwa na baba ake.
Nilimfuata dada mmoja jirani yangu ambae alikuwaga ananisaidia hela na chakula kila nilipokuwa naenda kumuomba
Nilipo mfuata kuomba ushauri nifanye nini, nilimuelezea historia yangu yote kuanzia mume alietaka kuniona wakati bado nipo msichana kisha akaingia mitini kabla ndoa haijafungwa, mwanaume nilie zaa nae mtoto wa kwanza, wapili hadi huyu ambae amefariki na kuniacha na kichanga cha miezi minane.
Dada huyu akaniambia atasaidia kunihudumia hadi nitakapo nijifungua na nikisha jifungua atanipeleka kwa mganga ambae atanisaidia.
Kweli alifanya kama alivyo niahidi. Bahati mbaya mtoto hakuwa riziki. Alizaliwa akiwa amefariki tayari.
NAPELEKWA KWA MGANGA
Tulipofika kwa mganga akanitazama na kuniambia kuwa nimefungwa kichawi.
Mganga akaniambia kuwa nyota yangu iliibwa kichawi muda mrefu kwa ajili ya kwenda kutumikishwa kichawi.
Mganga akaniambia hakuna haja yoyote ile ya kuirudisha nyota hiyo kwa sababu imeshakufa huko ilipo na haiwezi kunisaidia kitu chochote hata kama itarudishwa kwa sababu imetumikishwa .
Akaniambia ilikuwa niolewe tangu nikiwa na miaka 20,lakini “ndoa” yangu ilibatilishwa kichawi kwa kutumia bundi na bahati yangu ya kuolewa akapewa mwanamke mwingine.
Na kweli kwa mujibu wa kumbukumbu zangu, nikiwa nina umri huo kuna mwanaume mmoja alitaka kunioa lakini badae ndoa ikapeperuka hata sijui kitu gani kilitokea.
Mganga akaniambia kwa kuwa bahati yangu ya ndoa iliibwa kwa kutumia bundi basi na mimi itabidi niibe bahati ya mtu mwingine kwa kutumia bundi.
Sikuwa na jinsi Zaidi ya kukubaliana na mganga pamoja na kwamba sikujua lingewezekanaje hilo..
NAAMBIWA NIKACHUME MTI WA PILIPILI NIKIWA KWENYE SIKU ZANGU.
Mganga akaniambia nirudi nyumbani, halafu siku nitakapo ziona siku zangu basi niende kwenye mti wa pilipili nichume pilipili halafu niutazame vizuri huo mti kisha nimjulishe nimeona nini.
NACHUMA MTI WA PILIPILI NIKIWA KWENYE SIKU ZANGU
Siku nilipoziona siku zangu nikaenda kuchuma pilipili. Niliona kitu cha ajabu sana. Kitu ambacho sikuwahi kukiona tangu nizaliwe.Ule mti wa pilipili ulikauka ghafla. Niliogopa sana nikampigia mganga. Mganga akaniambia niuchume huo mti halafu kesho niende nikamuone.
NAPELEKA KWA MGANGA MTI WA PILIPILI ULIO KAUSHWA NA HEDHI
Kesho yake nikadamkia kwa mganga na mti wa pilipili ulio kauka. Mganga akauchukua huo mti na kuusaga pamoja na dawa zake nyingine anazo zijua yeye mwenyewe. Baadae akanichanja akanipaka mafuta ambayo sikujua ni mafuta ya nini. Akanipa dawa za kuoga, na kunywa pamoja na hirizi.
Halafu akanipa dawa ya kuchoma usiku.
MGANGA ANANIELEKEZA NAMNA YA KUWAITA BUNDI NA KUWASILIANA NA BUNDI KWA ISHARA.
Mganga akaniambia haya mafusho ninayo kupa ni uchawi mkubwa sana.
Zingatia masharti yote nitakayo kupa vinginevyo utapata madhara makubwa sana.
Akaniambia hilo ni fusho maalumu la kuwaita bundi. Kwa kutumia fusho hilo utakuwa unawaita bundi na kwa kuwatumia bundi hao utaweza kujua ni katika nyumba gani kuna mwanamke mwenye bahati ya kuolewa.
Kupitia bundi utaweza kujifunza vitu vingi sana ambavyo ulikuwa hauvijui.
Mbali na kujua mwanamke gani ana bahati ya kuolewa, unaweza kujua kwenye nyumba gani kuna watu wana nyota nzuri nakadhalika.
Mganga akaniambia nitakufundisha namna ya kutafsiri ishara mbalimbali za milio ya bundi.
i. Bundi akilia mara moja, anatoa ishara kuwa katika nyumba hiyo kutatokea msiba hivi karibuni. Na hapo itategemea amelia saa ngapi. Kama akilia kati ya saa sita na saa saba usiku basi anakuwa anatoa ishara ya kutokea kwa msiba na kama kama atalia kati ya saa 4 na saa 5 usiku anakuwa anatoa ishara na kuwaonya wenye mji juu ya ujio wa wachawi katika mji huo usiku huo.
Hii ni kwa sababu bundi anaweza kuona mambo ya sirini, mambo aliyo fichwa mwanadamu na mambo yatakayo tokea siku za mbeleni.
ii. Bundi akilia mara mbili maana yake ni kwamba wewe ulie isikia sauti hii utapata mafanikio makubwa sana katika kitu unacho taka kukianzisha hivi karibuni, na ili ufanikiwe katika kitu au jambo hilo ni lazima ukifanye haraka iwezekanavyo.
iii. Bundi akilia mara tatu basi anatoa ishara kwamba katika nyumba iliyopo karibu na mti ambao bundi huyo alitua wakati analia, kuna mwanamke ataolewa na ndoa yake itadumu kwa muda mrefu.
iv. Bundi akilia mara nne anakuwa anatoa ishara kwamba wakaazi wa nyumba au mtaa huo watapata usumbufu mkubwa katika siku za karibuni.
v. Bundi akilia mara tano anatoa ishara kwamba wewe ulie sikia sauti hiyo utapata safari nzuri hivi karibuni.
vi. Bundi akilia mara sita anatoa ishara kwamba, kuna wageni wapo njiani wanakuja kuwatembelea.
vii. Bundi akilia mara saba anatoa ishara kwamba kuna mtu au watu katika nyumba hiyo watapatwa na matatizo ya msongo wa mawazo.
viii. Bundi akilia mara nane, anakuwa anatoa ishara kwamba katika nyumba hiyo utatokea msiba wa ghafla.
ix. Bundi akilia mara tisa anatoa ishara ya bahati njema katika nyumba hiyo.
Sasa basi, wachawi huwa wanakuwa makini sana kusikia sauti za bundi pindi wanapolia. .
Baada ya hapo mganga akaniambia natakiwa kwenda kumwaga mafusho hayo kidogo kwenye mti wowote mkubwa ulio jirani na nyumba ambayo nimeikusudia na kuchukua jani la huo mti kwenda nalo hadi chumbani kwangu kisha kulichoma kwenye chetezo pamoja na hayo mafusho huku nikitamka maneno maalumu ya kuwaita bundi waje kwenye huo mti ili waweze kujua ni mwanamke gani anakaribia kuolewa ndani ya nyumba hiyo.
Usiku wa siku hiyo nikafanya kama nilivyo elekezwa. Nikaenda kuchuma jani la huo mti na kuwamga fusho kidogo kwenye mti kisha ilipofika saa tatu za usiku nikaanza kuchoma ilo fusho pamoja na jani la huo mti.
Ilipofika saa sita usiku kweli bundi wakaja na muda si mrefu wakaanza kulia. Nikasikia kwa makini sana.
Bundi akalia mara tatu . Alilia kutoka kwenye mti uleule ulio jirani na nyumba ya shangazi yangu. Nilichagua mti ulio jirani na nyumba ya shangazi yangu kwa sababu shangazi yangu alikuwa na watoto wengi wa kike na nyumba yake ilikuwa na wageni na wapangaji wengi wanawake.
Mganga aliniambia bundi wakisha nyamaza tu nimjulishe haraka sana.
Kama alivyo nielekeza mganga nikamjulisha.
Nilipo mjulisha akaniambia sawa, nilale halafu kesho asubuhi nihakikishe naenda kwa shangazi yangu au naongea na mtu yoyote anaeishi nyumbani kwa shangazi yangu.
Nitakapo kuwa hapo kwa shangazi yangu nisikie kama watazungumza chochote kuhusu bundi na kama wasipo zungumza basi nijifanye kuanzisha mazungumzo kuhusu bundi, nijifanye na mimi jana bundi walitua nyumbani kwetu na kwamba ninaogopa sana.
Na watakacho nijibu basi nimjulishe mganga.
Kweli nikaenda hadi kwa shangazi na bahati nzuri nikamkuta binamu yangu ambae ndio nilibatilisha ndoa yake kichawi.
Binamu hakuwa na dalili zozote za kupiga story kuhusu bundi hivyo nikaanzisha story za bundi kwamba jana bundi walilia sana batini kwangu na kwamba nilishindwa kulala.
Binamu akaniambia hata kwao ilikuwa hivyo hivyo na sio kulia tu bali kuna wakati bundi waliingia hadi ndani wakatua na kuondoka.
Tukaongea kwa muda kidogo kisha baada ya hapo nikampigia mganga na kumueleza kila kitu.
Mganga akaniambia vizuri sana, mambo yako yatakuwa mazuri sana.
Niseme kitu kimoja, wachawi kwa kumtumia bundi, wakishajua kwenye nyumba Fulani kuna mtu ana nyota ya kuolewa hivi karibuni au kuna watu wenye nyota kali wamelala kwenye nyumba hiyo huwa wanawatuma bundi kwenda kuiba nyota hizo.
Hivyo basi siku ukisikia bundi wamelia mara tatu karibu na nyumba yenu halafu baadae wakaingia ndani basi jua bahati ya kuolewa ya mtu imeibiwa na kama kuna watu wenye nyota kali walikuwa ndani ya nyumba hiyo basi na nyota zao zinakuwa zimechukuliwa pia.
Hivyo ndivyo alivyo niambia Dokta na akaniambia ikitokea nimeenda kwenye mji wa ugenini halafu jambo hilo likatokea, basi nihakikishe huyo bundi atakae ingia ndani anauliwa au anakamatwa kabla hajapaa,jambo ambalo hata hivyo ni gumu sana kwa sababu bundi wanapo ingia ndani huwezi kuwasikia kwani huwa wanapaa bila kupiga kelele wala kutoa sauti.
Dokta akaniambia huu ni uchawi unao tumika sana na hautumiki kwenye masuala ya mapenzi tu bali biashara pia.
Akaniambia wafanya biashara wengi wametajirika na wanaendelea kutajirika kwa kutumia uchawi huu wa kuiba nyota za watu kwa kuwatumia bundi.
Na hii ndio sababu bundi anatukuzwa sana miongoni mwa wafanya biashara.
Mganga akaniambia ili nyota isichukuliwe na bundi kwa staili hiyo natakiwa niwe na kinga maalumu ya kuwazuia bundi kuchukua nyota.
Akasema kinga hii ni tofauti na kinga zingine zote na kwamba hata kama una kinga nyingine yoyote ile lazima kinga hii uwe nayo pia.
Akaniambia kwa kuwa nimeingia kwenye mtandao huu inabidi hiyo kinga niwe nayo.
Siku ya kutengeneza kinga hii,mganga alichukua paka mweusi, akauliwa kisha akatobolewa macho halafu kwenye macho yake zikawekwa mbegu za mti wa mnyonyo kila jicho.
Paka huyo akafungwa kwenye kitambaa cheupe mfano wa maiti akawekwa kwenye mfuko nikapewa kwenda nae na kumzika vichakani kwenye eneo ambalo nitaliweka alama… Nikawa namwagilizia maji kila siku hadi mti ulipo chipuka na kukua.. Mti ulipo kua mganga akaniambia nitoe mbegu, nikafanya kama alivyo nielekeza . Mganga akaniambia nichukue mbegu saba kisha nimpelekee.
Nilipo mpelekea mbegu hizo mganga, akazichukua akachanganya na dawa zake anazo zijua mwenyewe akachukua popo,akamkata kucha akiwa hai na kumuacha, akaziasaga na muzichoma kisha kunichanja na kunipaka.
BAADA YA BUNDI KULIA NA KUTUA KWENYE NYUMBA YA SHANGAZI YANGU
Sikuwa najua kama binamu yangu mtoto wa shangazi yangu alikuwa na mpango wa kuolewa kwa sababu ni jambo lililofanywa siri.
Lakini siku chache baada ya bundi kutua kwenye nyumba ya shangazi yangu nikaanza kusikia habari za kuharibika kwa mipango ya ndoa ya binamu yangu.
Binamu yangu alitaka kujaribu kujiua baada ya mume mtarajiwa kugombana nae na kuingia mitini na kisha kuhamishia uchumba kwa mwanamke mwingine.
Wakati huo huo,mimi nikapata mwanaume mwenye pesa ambae alinichumbia na kunioa tena kwa harusi kubwa.
Ni hivi bahati ya ndoa ya mtu inayo ibwa kwa kutumia bundi, sio lazima wewe uolewe na aliekuwa anataka kumuoa mwanamke uliye iba bahati yake.HAPANA. Ni hivi inaweza kutokea mwanaume huyo labda akafukuzwa kazi ghafla au akafilisika na mipango yake kuvurugika.
Nyota ya mwanaume huyo inaibwa anapewa mwanaume mwingine ambae atakuja kukuoa wewe.
NAAMUA KUACHANA NA USHIRIKINA NA KUMRUDIA MUNGU.
Niliishi na mwanaume huyo toka 2014 hadi 2016 katikati.. Siku moja nilipokea taarifa za msiba wa rafiki yangu ambae ndio aliniunganisha na huyo mganga.
Huyu dada alikuwa anaishi maisha ya kidini lakini kumbe alikuwa anafanya ushirikina sana.
Kuhusu kifo chake, sijui kama kilitokana na ushirikina ama ni mipango ya mungu lakini nilipo ona mwili wake niliogopa sana.
Niliwaza nakuwazua, nilitafakari nakutafakari. Nikajiuliza moyoni kumbe na mimi pamoja na mali na pesa hizi nilizo zipata kwa njia ya ushirikina ipo siku nitakuwa kama huyu ?
Kumbe mimi sio kitu kabisa katika dunia hii ? Kumbe binadamu ni mchanga.
Kumbe binadamu ananuka na kutoa harufu ? Kumbe ipo siku ndugu zangu wataogopa kulala na mimi ?
Nilitakafakari sana .. Nilikumbuka mambo mengi ya utotoni. Jinsi nilivyo lelewa na wazazi wangu.
Nililelewa kufuata maadili ya Mungu na kuwa mvumilivu na mstahimilivu kwa namna yoyote ile.
MAHUBIRI YA MCHUNGAJI WAKATI WA MAZISHI YANILIZA
Nikiwa katika hali ya majuto na uchungu mkubwa Mchungaji alianza kuhubiri neno la Mungu.
Alihubiri mambo mengi sana lakini kikubwa aliwasisitizia waombolezaji kumkumbuka Mungu wakati wa uhai wao na kwamba hapa duniani tunapita tu.
Mchungaji waliwaasa waumini wasiwe na tamaa na mali za duniani hapa kwani tutaziacha hapahapa duniani.
Mchungaji akawakumbusha waumini kwa kuwasomea neno la Mungu kutoka katika kitabu cha MATHAYO 16 : 26 ambalo linasema
“Kwa maana mtu atapata faida gani akiupata ulimwengu wote lakini aipoteze nafsi yake?au mtu atatoa nini ili aipate nafsi yake?”
Hapa Mchungaji akawa kama ananiongelea mimi kabisa.
Baadae akasema najua kuna watu wanakata tamaa ya kufanikiwa katika maisha kwa sababu wamehangaika muda mrefu bila mafanikio.
Shetani anazitumikisha nafsi zao kwa faida yake na watu wake. Wametupiwa nuksi na mikosi na wachawi.
Mungu anasema katika kitabu cha YOELI 2 Sura ya 25 Nami nitawarudishia hiyo miaka iliyoliwa na nzige, na parare, na madumadu, na tunutu, jeshi langu kubwa nililotuma kati yenu…
Baadae Mchungaji akasema kama kuna watu wapo tayari kuokoka basi na wanyooshe mikono yao nami nitawaongoza sara ya toba.
Nilidhani ni mimi tu nitakae nyoosha mkono wangu lakini nilishangaa kuona na watu wengine wengi tu wakinyoosha mikono yao.
Hata yule binamu yangu ambae niliiba nyota yake kichawi nae alinyoosha mkono wake. Wote tuliombewa na baadae tukaanza mafundisho kanisani na hadi muda huu ninaondika waraka huu bado tunaendelea kumtumikia Mungu.
KUHUSU MUME WANGU : Mume wangu alinikimbia baada ya kuona nimeokoka jambo ambalo nililishukuru pia kwa sababu hakuwa haki wala staili yangu.
MAISHA YETU YA MAHUSIANO KWA SASA.
Kwa sasa mimi nina mchumba na yule binamu yangu ameshaolewa tayari.
KUHUSU MGANGA ALIYE NIINGIZA KWENYE SUALA LA KUIBA NYOTA ZA WATU KWA KUMTUMIA BUNDI.
Mganga huyu anajulikana Zaidi kama mungu wa kabili na namba zake za simu ni 0744 -000 473.
NIMEWEKA JINA LAKE NA NAMBA ZAKE ZA SIMU ILI WATU WAJUE KWAMBA HUYU NI MCHAWI NA WAKALA WA WACHAWI NASHETANI NA WAEPUKANE NAE KWA SABABU ATAWAINGIZA KWENYE MAMBO YA UTUMWA WA ULOZI NA UCHAWI KAMA ALIVYO FANYA KWANGU.

Post a Comment

1 Comments

  1. Karibu Tiba asili na Dokta, Mdirokupata tiba mbalimbali kupitia visomo na dawa mbalimbali..

    PIGA SIMU No, 0742162843...

    Kwa wale wasumbuliwao na magonjwa sugu na matatizo kama
    Kusafisha nyota, biashara, kumvuta mpenzi, KUTENGENEZA MALI KWA NDAGU au KUTENGENEZA MALI KWA MAJINI, kulinda mali, kulinda familia, Utulivu katika ndoa, kuitambua nyota yako, Kwa wale wasumbuliwao na majini(mapepo) na mengine mengi kumbuka husitume sms tafadhali piga simu kuhepuka matapeli.

    KUMBUKA MALIPO NI BAADA YA KUFANIKIWA KWA MASWALA YA KUPATA PESA ZA NDAGU AU MAJINI......

    piga namba +255742162843

    (KWANINI USUMBUKE,HACHA KUTANGATANGA, NA MAISHA NI MAFUPI PUUZA UONGOFU WA KUWA MTU KUWA TAJIRI NI DHAMBI WAKATI AKUAMBIAE YEYE NI TAJIRI...

    Naitwa Dokta Mdiro, piga simu 0742162843 kwa maelezo zaidi...

    UTAJIRI WA NDAGU(MASHARTI) NDANI YA MASAA 72(SIKU TATU) PAPO HAPO KIKUBWA UWE MWAMINIFU, JASILI NA UWE NA UTAYARI WA KUPOKEA MASHARTI YA KUTUNZA SIRI HII SIO MZAHA......

    (kuhusu utajiri au pesa) KABLA YA KUPIGA SIMU ZINGATIA YAFUATAYO
    1. uwe una umri wa miaka 18+
    2. uwe tayari kupokea masharti yote
    3.uwe na uwezo wa kutunza siri
    4. uwe jasiri wa kupokea taarifa yoyote
    KARIBU SANA KWA SHIDA NYINGINE PIA ULIYONAYO AMBAYO SIJATAJA INSHAALAH ITATATULIWA IKIWA NDANI YA UWEZO WANGU.

    ReplyDelete