Waziri wa
Mifugo na Uvuvi, Luhaga Mpina ametangaza kupiga mnada ng'ombe zaidi ya 10,000
wa nchi za Uganda na Rwanda waliokamatwa katika operesheni inayoendelea nchini.
Mpina
alitangaza hayo leo Jumatatu bungeni mjini Dodoma wakati akichangia Mpango wa
Taifa wa Maendeleo wa 2018/2019.
Waziri huyo
ambaye alikuwa akijibu hoja zilizoibuliwa na baadhi ya wabunge amesema ng'ombe
hao watapigwa mnada wakati wowote kama ilivyofanya kwa ng'ombe 1,325 wa Kenya.
Amesema
uhusiano wa Tanzania nchi nyingine washirika wa Jumuiya ya Afrika Mashariki
(EAC) ni mzuri na akisisitiza hakuna ushirikano wa kihalifu.
Mpina
amesema walioingiza ng'ombe hao ni wahalifu na wamevunja sheria za nchi na
kutahadharisha wafugaji wa nchi jirani kufuata sheria wanapotaka kuingiza
mifugo nchini.
0 Comments