Follow us

Jeshi la Zimbabwe: Tunawalenga wahalifu

Tangazo
Jeshi la Zimbabwe limesoma taarifa kwenye kituo cha runinga cha serikali ZBC, likisema kuwa linachukua hatua ya kuwalenga wahalifu.

Hata hivyo limesema kuwa hayo sio mapinduzi ya kijeshi na Rais Mugabe yuko salama.
Milio mikubwa ya risasi ilisikika katika maeneo ya kaskazini mwa mji mkuu Harare mapema leo.
Taarifa hiyo ya jeshi ilikuja saa kadhaa baada ya jeshi kudhibiti kituo cha ZBC.

Mwanamume mmoja ambaye alikuwa amevaa sare za jeshi alisema kuwa jeshi linataka kukabiliana na watu ambao wanatenda uhalifu unaoleta madhara ya kijamii na kiuchumi nchini Zimbabwe.
"Wakati tutakapomalzia wajibu wetu, tunatarajia kuwa hali itadudi kuwa sawa."

Taarifa hiyo ilisema kuwa Mugabe 93, na familia yake wako salama.

Haijulikani ni nani anaongoza hatua hiyo ya kijeshi.
Magari ya wanajeshi waliojihami kwa silaha yameonekana maeneo ya mjini Harare.
Hali hiyo ya wasi wasi wa lolote kuweza kutokea, imeanza hapo jana jioni, ambapo wanajeshi wakiwa na silaha walionekana wakijipanga katika maeneo kadhaa pamoja na kuzingira ofisi za shirika la utangazaji la Zimbabwe ZBC.

Post a Comment

0 Comments