Follow us

GAMONDI MASTA NA HESABU KIMATAIFA HAPA

Tangazo



MIGUEL Gamondi, Kocha Mkuu wa Yanga amebainisha kuwa mpango mkubwa kwenye mechi za kimataifa ni kupata ushindi wapo tayari kutokana na maandalizi ambayo wanayafanya kwenye uwanja wa mazoezi.

Machi 30 Yangainatarajiwa kukabiliana na Mamelodi Sundowns mchezo wa Ligi ya Mabingwa hatuaya robo fainali Ligi ya Mabingwa Afrika.

Mchezo wao uliopita kwenye ligi Yanga ilipoteza kwa kufungwa mabao 2-1 dhidi ya Azam FC huku wachezaji wake wawili wakipata maumivu ikiwa ni Pacome Zouzoa na Yao Atohoula ambapo kwa sasa wanaendelea vizuri baada ya kupewa matibabu.

Kocha huyo amesemakuwa kwenye mechi za kimataifa ambacho kinahitajika ndani ya uwanja ni ushindijambo ambalo wanalifanyia kazi kwa kuzungumza na wachezaji na kufanyia kazimakosa yaliyopita kwenye mechi zao.

“Mechi za kimataifa zina utofauti wake hilo lipo wazi na tumekuwa tukifanya maandalizi mazuri kwa ajili ya kupata matokeo chanya kwenye mechi zetu ambazo tutacheza na tunatambua kamba wapinzani wetu wanahitaji ushindi kama ambao sisi tunautafuta.

“Mashabiki wanapokuwapamoja nasi wanaongeza nguvu kubwa hivyo waendelee kuwa nasi katika mechi zotetuna amini tutaendelea kutoa burudani ndani ya uwanja

Post a Comment

0 Comments