WABABE wa kundi F, lililokuwa na timu ya taifa ya Tanzania Taifa Stars iliyoishia hatua ya makundi, Morocco wamefungashiwa virago katika Kombe la Mataifa Afrika, (AFCON) mbele ya timu ya Afrika Kusini.
Baada ya dakika 90 ubao ulisoma Morocco 0-2 Afrika Kusini kwenye mchezo
wa hatua ya 16 bora.
Mabao yalifungwa na Evidence Makgopa dakika ya 57, Teboho Mokoena dakika
90+5.
Ngoma itakuwa ni dhidi ya Cape Verde katika hatua ya robo fainali, Ivory
Coast.
Wababe hao wamekutana na maajabu ya Afrika Kusini kwa kufungashiwa
virago mapema walipokuwa wakipewa nafasi ya kufanya vizuri kwenye AFCON 2023.
0 Comments