Follow us

Tetesi za Soka Ulaya Jumamosi 12.01.2019: Coutinho, Willian, Higuain, Shelvey, Casilla

Tangazo
Philippe Coutinho(kushoto)

Barcelona imesema iko tayari kupokea ofa ya kumnunua kiungo wao wa kati Philippe Coutinho, 26.

Manchester United imeonesha nia ya kumsaini mchezaji huyo wa zamani wa Liverpool wakati wa msimu wa joto. (Calciomercato, via Star)

Barcelona pia wameweka dau la pili la kumnunua winga wa Chelsea na Brazil, Willian, baada ya ofa yao ya kwanza ya kumnunua kiungo huyo wa miaka 30 kugonga mwamba siku ya Alhamisi. (Standard)

Chelsea imekubali kuwanunua kwa masharti viungo wa kati Nicolo Barella, kutoka klabu ya Cagliari na Leandro Paredes, 24, wa klabu ya Zenit St Petersburg. (Telegraph)




Neymar (kushoto)
Meneja wa AC Milan Gennaro Gattuso amesema kuwa klabu hiyo inaendelea kuzungumza na wawakilishi wa mshambuliaji Gonzalo Higuain licha ya tetesi kuwa mshambuliaji huyo huenda akahamia Chelsea. (Express)


Kumsaini kwa mkopo Higuain hadi mwisho wa msimu huu ndio mpango wake wakati huu wa uhamisho wa wachezaji. (Sun)

Baba yake Neymar ambaye ni nyota wa kamtaifa wa Brazil na Paris St-Germain amepinga uvumi kuwa nyota huyo wa miaka 26 anataka kurejea katika klabu yake ya zamani Barcelona. (Express)

Liverpool na Fulham wote wanataka kumsaini mshambuliaji wa Red Bull Salzburg na Israel Moanes Dabour, 26. (Estadio Deportivo - in Spanish).


Paul Pogba




Juventus wana mpango wa kumsaini tena Paul Pogba, 25, Manchester United endapo winga wa Brazil Douglas Costa, 28, atahamia Old Trafford kama sehemu ya mpango huo. (Tuttosport, via Calciomercato)


Juventus pia wako tayari kumuachilia beki wa kati wa Morocco Medhi Benatia, 31, kuenda Arsenal katika hatua ambayo itamwezesha Aaron Ramsey, 28, kuhamia upande wowowte. (Gazzetta dello Sport, via Metro)

Wolves wazidi kushangaza miamba, wawalaza Liverpool
Barcelona wanatafakari uwezekano wa kumchukua mshambulaji wa Chelsea na Uhispania Alvaro Morata, 26 kwa mkopo.

Morata huenda akanunuliwa na Sevilla na Atletico Madrid. (Sport - in Spanish)

Nahodha wa Arsenal Laurent Koscielny, 33, amekataa ombi la Monaco la kutaka ajiunge nao. (Le10 Sport, via Mirror)

chanzo BBC

Post a Comment

0 Comments