Follow us

Waziri Mkuu Awanusuri Vigogo vyama vya ushirika Kwenda Rumande

Tangazo

Vigogo wa Chama cha Ushirika mkoa wa Shinyanga (Shirecu), wa Chama cha Ushirika mkoa wa Mwanza (Nyanza) wameponea chupuchupu kuwekwa ndani na Waziri Mkuu Kassim Majaliwa kutokana na kutajwa kuwa miongoni mwa viongozi waliohusika kuuza mali za ushirika.
Akizungumza kwenye mkutano wa wadau wa zao la pamba uliojumuisha mikoa 16 ya Tanzania bara jana Desemba 22, Waziri Majaliwa alitaka kumuiagiza Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, Simon Haule kuwakamata vigogo hao.
Hata hivyo, aliwapa muda hadi Januari 13, mwakani wafike ofisini wake wakiwa na nyaraka zinazoonyesha mali za ushirika zilipo.
Alisema wamepoteza mali nyingi kwenye ushirika wa Nyanza likiwemo jengo la usafirishaji na viwanja ambavyo vimechukuliwa na watu wasio wanachama.
Alisisitiza kuwa watakapofika ofisi kwake wawe na maelezo kamili ya zilipo mali hizo, kama ziliuzwa waliouziwa wafike na nyaraka zinazoonyesha waliuziwa na nani.
“Nilitaka kumwambia RPC aondoke na nyinyi lakini ninawapa nafasi kila mmoja aje na maelezo ya zilipo mali na kama zimeuzwa hao waliouza waseme waliuziwa na nani," alisema na kuongeza,
"Tukutane siku hiyo ofisini kwangu saa 3 asubuhi. Lazima tuhakikishe mali hizi zinapatikana ili ushirika uendelee kuwa imara."
Miongoni mwa vigogo hao zaidi ya 13, wamo waliokuwa wahasibu ambapo upande wa Shirecu yumo pia meneja wake wa mkoa, Joseph Mihangwa na James Kusekwa.

Majaliwa alisema Shirecu inadaiwa Sh11 bilioni walizokopa Benki ya TIB pamoja na Sh 1.2 bilioni wanazodaiwa na wafanyakazi.

Post a Comment

0 Comments