Mchungaji
Jackson Sosthenes amechaguliwa kuwa askofu wa Kanisa la Anglikana Dayosisi ya
Dar es Salaam kwa kura 110 kati ya 185 zilizopigwa na wajumbe wa sinodi wa
kanisa hilo.
Mchungaji
Sosthenes amemshinda Mchungani Patrick Bendera aliyepata kura 74, huku moja
ikiharibika.
Uchaguzi huo
umefanyika leo Jumamosi Desemba 23,2017 katika Kanisa Kuu la Anglikana Dayosisi
ya Dar es Salaam la Mtakatifu Albano lililopo Posta wilayani Ilala jijini Dar
es Salaam.
Ofisa habari
wa dayosisi hiyo, Yohana Sanga amesema uchaguzi umelenga kumpata askofu wa tano
wa Dayosisi ya Dar es Salaam anayechukua nafasi ya Dk Valentino Mokiwa.
Amesema
walioshiriki uchaguzi huo ni wajumbe wa sinodi ambao ni mapadri, mashemasi,
walei, wajumbe wa vikao vya sinodi na wa idara katika dayosisi.
"Baada
ya Dk Mokiwa kuamriwa kujiuzulu nafasi hii ilishikiliwa na kasisi mkuu, Jerome
Napera ambaye leo amemkabidhi Canon Sosthenes,” amesema.
0 Comments