Askofu
Gwajima amesema hayo leo Jumatatu Desemba 25,2017 akihubiri katika ibada ya
Krismasi. Amesema anayeanzia juu ipo siku atashuka chini.
Amesema kwa
kawaida mafanikio ya mwanadamu yeyote duniani ni lazima yaanzie chini.
"Hata
Yesu alizaliwa kwenye hori la ng'ombe, sehemu ya chini kabisa lakini ndiye
aliyetukomboa na dhambi. Ogopa kilichozaliwa kwenye hori, ukiona mtu ameanzia
juu jua kuna siku atashuka," amesema.
Askofu
Gwajima amesema ingewezekana Yesu kuzaliwa sehemu ya heshima lakini Mungu
alitaka iwe hivyo kudhihirisha utukufu wake kwamba, kilichozaliwa kwenye hori
la ng'ombe ni kikuu.
Amesema
chochote kinachoonekana kinyonge na kidhaifu leo, kisidharauliwe kwa sababu ipo
siku kitaheshimiwa.
Akitoa mfano
amesema hata yeye alianzia chini kwa kuuza mihogo na barafu.
Amewatia
moyo waumini walio hatua ya awali ya maisha akiwataka kutokata tamaa kwa sababu
kuna wakati wa kuinuliwa.
"Niwaambie
tu msiogope, aliyeanza kwa udhaifu atamaliza kwa heshima," amesema.
Amewataka
kujenga tabia ya kuwasikiliza hata wale aliowaita waropokaji kwa sababu kuna
wakati Mungu anaweza kuwatumia wakawa na ujumbe wenye kujenga.
0 Comments