Follow us

Yanga SC wapatwa na msiba mzito

Tangazo
Klabu ya Yanga imepatwa na msiba mzito wa baba yake mzazi na kocha mkuu wa klabu hiyo, Mzambia George Lwandamina.

 Kocha wa Yanga, George Lwandamina

Taarifa hiyo  imethibitishwa na Afisa habari wa klabu hiyo Dismas Ten na kusema kuwa ni kweli kocha wao amepatwa na msiba wa baba yake mzazi huko kwao Zambia na tayari wameshafanya mpango wa kumsafirisha Lwandamina kwenda kuhudhuria msiba huo.

“Lwandamina ameondoka leo nchini Tanzania kuelekea nyumbani kwao Zambia kwa ajili ya mazishi ya baba yake, ila akifika huko ndiyo tutaweza kujua tarataibu za mazishi kwa kuwa shuguli zote zinafanyikia huko kwao”,.

Hata hivyo awali taarifa za kuondoka kwa kocha huyo nchini Tanzania zilieleza kuwa kuna matatizo ya kifamilia.

Singida Blog na laurentcomputercentre.com  inatoa pole kwa kocha Lwandamina na klabu ya Yanga kwa ujumla.

Na Laurent Mpoma

Post a Comment

0 Comments