Mkurugenzi Mtendaji wa Taasisi ya moyo ya Jakaya Kikwete,
Prof.Mohammed Janab ameielezea mahakama ya hakimu mkazi kisutu kuwa moyo wa
mfanyabiashara Yusuf Manji umewekwa vyuma ili kumsaidia kupumua.
Prof. Janab ambaye ni Daktari wa moyo na Shahidi wa kwanza
upande wa utetezi ameyasema hayo mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi, Cyprian Mkeha
wakati akitoa ushahidi katika kesi ya dawa za kulevya inayomkabili Manji ambapo
akiongozwa na Wakili wa utetezi, Hajra Mungula, alisema yeye ni Daktari wa moyo
wa Taasisi ya JKIC.
Amesema anamfahamu Manji baada ya kufikishwa katika Taasisi
hiyo February 2017 akiwa mwenye matatizo ya moyo na kuongeza kuwa alipofikishwa
hapo alifanyiwa vipimo na jopo la madaktari lililobaini Moyo wake umewekewa
vyuma ambapo akaingizwa mipira maalum na kubaini kwamba upo katika hali nzuri.
Alipoulizwa na Wakili Mungula kama mgonjwa aliyewekewa vyuma
katika moyo anaweza kutumia dawa za kulevya, Prof. Janab alijibu kwamba huwa
haruhusiwi kufanya baadhi ya mambo ikiwemo kuvuta sigara, kutumia Heroin.
“Hivyo kama akitumia athari zake ni kwamba mirija ya moyo
itaziba, kisha atatakiwa afanyiwe upasuaji mkubwa zaidi.”
Prof. Janab ameongeza kuwa katika awamu ya pili ya Manji
kurudi hospitalini hapo walimsaidia kumtibia maumivu aliyokuwa nayo kwa kumpa
Drip ya Paracetamol’s na Sindano ya Tram a do.
Akijibu hoja ya Wakili wa Serikali, Timony Vitalis kwamba
matumizi ya dawa za kulevya yanaweza kusababisha ugonjwa wa moyo, Prof. Janab
alijibu ndio.
Kesi imeahirishwa hadi August 31, 2017 kwa ajili ya
kuendelea na ushahidi.
0 Comments