Follow us

chini ya operesheni 1 kati ya 4 za misaada ndizo zimeruhusiwa Gaza.

Tangazo

 


Mamlaka ya Israeli imeendelea kuzuia misaada ya kuokoa maisha kufikia kaskazini mwa Gaza siku 102 tangu mashambulio ya ugaidi yaliyoongozwa na Hamas yaliposababisha vita, umesisitiza Umoja wa Mataifa akiwemo Katibu Mkuu António Guterres ambaye ameonya kwamba "Jinamizi la muda mrefu la njaa linawazogoma watu wa Gaza.”

 Ofisi ya Umoja wa Mataifa ya kuratibu misaada ya kibinadamu na masuala ya dharira OCHA imesema leo mjini Geneva Uswis kwamba "Katika wiki mbili za kwanza za Januari, ni asilimia 24 tu au operesheni 7 kati ya 29 zilizopangwa  kutoa msaada wa chakula, dawa, maji na vifaa vingine vya kuokoa maisha zilifanikiwa kufika kaskazini mwa Wadi Gaza".

 Akizingatia wasiwasi huo na kuangazia hali mbaya kila mahali kwenye eneo la Gaza linalokaliwa mfanyakazi wa OCHA Olga Cherevko amesema kuwa hali ni mbaya kwa watu waliotawanywa kusini mwa Gaza pia.

 "Watu wengine hawajala kwa siku kadhaa," amesema leo kwenye video aliyoiweka kwenye mtandao wake wa kijamii wa X, zamani wa Twitter na kuongeza kuwa "Watoto hawana nguo za msimu wa baridi. Hakuna huduma za matibabu na kiwango cha mahitaji ni kikubwa. "

 

Mafuta, dawa vimekataliwa kuingia

Katika taarifa yake ya hivi karibuni juu ya vita ambayo iliyotolewa Jumapili jioni, OCHA ilibainisha kuwa makao vitu vingi vilivyokataliwa na Israeli vinahusisha mafuta na dawa zilizotengwa kwa hifadhi, visima vya maji na vituo vya afya kaskazini mwa Wadi Gaza.

 

"Ukosefu wa mafuta kwa ajili ya kusukuma maji, usafi wa mazingira na usafi huongeza hatari za kiafya na hatari za mazingira. Ukosefu wa dawa umedhoofisha utendaji wa hospitali sita zinazofanya kazi kwa kiasi kidogo limesema shirika la OCHA na kuonyesha kuwa " Mashambulizi makali ya Israeli, angani, ardhi na baharini, kupmbana na na vikundi vyenye silaha vya Palestina yameendelea kughubika sehemu kubwa ya Gaza, huku makombora yanayovurumishwa na vikundi vyenye silaha vya Palestina kuingia Israeli  yakiendelea pia”.

 

Wakati huo huo, shirika la afya la Umoja wa Mataifa WHO limeripoti kwamba kituo cha afya cha Nasser Medical Complex katika mji wa kusini wa Khan Younis "kinaendelea kupata idadi kubwa ya wagonjwa wenye kiwewe na visa vya kuungua".

Mzigo mkubwa kupindukia

Kwa muji wa WHO hospitali hiyo ina wagonjwa 700 idadi ambayo ni mara mbili ya uwezo wake wa kawaida wakati kitengo cha ICU na  majeraha ya moto "hakina wafanyikazi wa kutosha na hivyo kuchelewesha matibabu ya kuokoa maisha".

Maendeleo hayo yamefuatoa ombo la kusitisha mapigano kwa pande zote lililotolewa Jumatatu na mkuu wa Umoja wa Mataifa Bwana Guterres.

Pia alitaka kuachiliwa mara moja na bila masharti ya mateka wote waliochukuliwa wakati wa shambulio la kigaidi la Oktoba 7 na uchunguzi kamili wa madai yote ya unyanyasaji wa kijinsia dhidi ya wanamgambo wa Palestina ufanyike.

"Hatuwezi kutoa misaada ya kibinadamu wakati Gaza iko chini ya milipuko mizito ya mabomu, iliyosambaa na isiyo na mwisho," Bwana Guterres alisema, huku alionyesha wasiwasi mkubwa juu ya uharibifu wa jumla na viwango vya majeruhi kwa raia ambacho si cha kawaida kwa kipindi chapote ambacho amekuwa Katibu Mkuu.

Guterres aliendelea kusema kwamba "Wakati kumekuwa na hatua kadhaa zilizopigwa katika kuongeza mtiririko wa msaada wa kibinadamu ndani ya Gaza, lakini bado kiasi cha misaada ya kuokoa maisha haijawafikia watu ambao wamevumilia miezi ya kushambuliwa katika kiwango kinachopaswa na kinachohitajika."

Hivyo amesema halii inasababisha "Kivuli cha muda mrefu cha njaa kuwaghubika watu wa Gaza sanjari na magonjwa, utapiamlo na vitisho vingine vya kiafya."

 

Post a Comment

0 Comments