Mabingwa wa Tanzania, Yanga Sc wamefufua matumaini ya kwenda Robó Fainali ya Mabingwa Afrika kufuatia ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Medeama ya Ghana Uwanja wa Benjamín Mkapa Jijini Dar es Salaam.
Mabao ya Yanga Sc yamefungwa na kiungo
Muivory Coast, Peodoh Pacome Zouzoua dakika ya 33, mshambuliaji Mzambia Kennedy
Musonda dakika ya 61 na kiungo mzawa, Mudathir Yahya Abbas dakika ya 66.
Pongezi kwa kipa wa Kimataifa wa Mali,
Djigui Diarra aliyeokoa mkwaju wa penalti wa Jonathan Sowah dakika ya 55
kufuatia mshambuliaji huyo wa Kimataifa wa Ghana huyo kuchezewa rafu na mlinzi
na Nahodha wa Yanga, Bakari Nondo Mwamnyeto.
Medeama ilimaliza pungufu baada ya Sowah
kutolewa kwa kadi nyekundu dakika ya 90 kufuatia kuonyeshwa kadi ya pili ya
njano.
Kwa ushindi huo, Yanga Sc inafikisha pointi
tano na kusogea nafasi ya pili, nyuma ya mabingwa watetezi, Al Ahly wanaoogoza
kwa wastani wa mabao wakiwa na mechi moja mkononi.
Medeama inashukia nafasi ya tatu ikibaki na
pointi zake nne za mechi nne pia nyuma ya CR Belouizdad ya Algeria yenye pointi
nne pia na wastani zaidi wa mabao wakiwa na mechi moja mkononi pia.
Mechi zijazo, Yanga Sc watakuwa wenyeji wa CR Belouizdad Februari 23, kabla ya kwenda kumalizia mechi za Kundi D Jijini Cairo dhidi ya Al Ahly Machi 1 mwakani.
0 Comments