Follow us

Sadio Mane: mchezaji wa kiungo cha mbele wa amekubali mkataba wa muda mrefu Liverpool

Tangazo
Sadio Mane

Mchezaji wa kiungo cha mbele wa Liverpool na timu ya taifa ya Senegal Sadio Mane amekubali mkataba wa muda mrefu kuendelea kucheza Anfield.

Mchezaji huyo mwenye miaka 26 alijiunga na klabu hiyo kutoka Southampton kwa mkataba wa miaka 5 mnamo Juni 2016 kwa thamani ya £ milioni 34.

Tangu hapo amecheza mara 89 katika mashindano yote ya timu hiyo ya Jurgen Klopp na kufanikiwa kufunga magoli 40.

"Ninafurahia sana kurefusha muda wangu Liverpool. Ni siku nzuri mno kwangu na huu ni uamuzi bora kabisa katika kazi yangu," amesema.



Mazungumzo kuhusu mkataba huo unaodumu hadi 2023, yaliidhinishwa mwishoni mwa msimu uliopita lakini yamekamilishwa hivi punde tu.

"Natazamia kila kitu - kuisaidia timu, kuisaidia klabu kutimiza ndoto yetu hususan kushinda mataji," aliongeza.

"Daima nimekuwa nikisema, nilipojuwa nina nafasi kuja hapa sikufikiria mara mbili. Klabu muafaka, kwa wakati muafaka, kwa kocha aliye sawa. Nilikuja hapa na nilifurahi sana.."


Sadio Mane

Mane alipigiwa kura kuwa mchezaji bora wa timu hiyo na mchezaji bora wa wachezaji katika msimu wake wa kwanza na baadaye akafunga magoli 10 kati ya yake 20 msimu uliopita katika ligi ya mabingwa wakati Liverpool ilipofika katika fainali.

Aliichezea timu ya taifa ya Senegal katika mashindano ya kombe la dunia 2018 nchini Urusi na kufanikiwa kufunga mara moja katika mechi tatu za nje.



Hivi karibuni ametajwa katika orodha ya wachezaji 30 kwa tuzo ya Ballon d'Or na ni miongoni mwa wagombea watano wa tuzo ya mchezaji bora wa soka wa BBC Afrika mwaka huu.

"Siwezi kufikiria klabu yoyote Ulaya ambayo haiwezi kumtaka mchezaji kama Mane awachezee, kwahivyo kwamba anataka kuendelea kucheza na sisi, inatoa ujumbe kuhusu sehemu tuliopo kwa sasa," amesema meneja wa Liverpool, Klopp.

Mkataba wa Mane unafuata mikataba mingine kama hiyo ya muda mrefu kwa wachezaji wenzake Mane wa kiungo cha mbele, Roberto Firmino, aliyekubali mkataba huo mnamo Aprili, na Mo Salah, aliyesaini mkataba mpya Julai.

Post a Comment

0 Comments