Follow us

Diamond amtambulisha msanii mpya wa WCB

Tangazo







Mwimbaji kutoka WCB ambaye anafanya vizuri katika mziki wa Bongofleva Diamond Platnumz kupitia Clouds 360 ya Clouds TV amemtambulisha msanii mpya ambaye atakuwa mmoja kati  ya wasanii wanaounda kundi hilo.

Katika utambulisho huo Diamond amesema kuwa ana wajibu mkubwa wa kuwasaidia wengine kwa kuwa hata yeye alisaidiwa ndiyo maana amefikia hatua hiyo aliyofikiwa.


“Ujio wangu hapa leo ni kwa ajili ya kumtambulisha kijana wetu mwingine kama sehemu ya kuwasaidia wengine. Nawashukuru sana Clouds Media kuwa kama daraja kuwasaidia wengine. Kama nisingesaidiwa nisingefika hapa. Inapotokea mtu anasaidiwa nashiriki kwa kidogo nilichonacho kwa sababu mimi nisingesaidiwa nisingefika hapa”.

Post a Comment

0 Comments